Tuesday, September 25, 2012

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KATIKA kusimamia uongozi unaozingatia misingi muhimu ya haki za binadamu, sheria na utawala bora, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesisitiza msimamo wake wa kutotoa ushirikiano kwa kamati iliyoundwa na Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi kuchunguza kifo cha Mwandishi wa Habari wa Channel ten, Daudi Mwangosi, kilichotokea Septemba 2, 2012, Kijiji cha Nyololo, mkoani Iringa.

Msisitizo huo umekuja baada ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo kukiandikia barua (isiyokuwa na Kumbukumbu Namba) CHADEMA, akiomba kamati yake ikutane na viongozi wa chama Septemba 25, ili kutafakari tukio hilo na matukio ya aina hiyo yaliyowahi kutokea hapa nchini.

Itakumbukwa kuwa Marehemu Mwangosi aliuwawa na Jeshi la Polisi akiwajibika kwa jamii katika shughuli za uandishi wa habari, wakati askari wa jeshi hilo walipovamia ofisi za CHADEMA Kata ya Nyololo na kuanzisha vurugu wakati wanachama walipokuwa wakiendelea na shughuli halali za ndani za chama.

Katika barua kwenda kwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, CHADEMA kimesema wazi kuwa hakiko tayari kukaa na kutafakari juu ya kifo cha Mwangosi kama ilivyopendekezwa na kamati hiyo, kwani haipo kwa mujibu wa sheria, huku pia ikiwa imeundwa na mtu ambaye kanuni za msingi za utawala bora, zinamtaka awe amejiuzulu au kufukuzwa kazi, kupisha uchunguzi huru juu ya mauaji hayo yaliyofanywa na jeshi la polisi, linalowajibika kwake kama Waziri wa Mambo ya Ndani. Kamati hiyo pia inawahusisha polisi ambao katika tukio hilo ni watuhumiwa namba moja.

Mbali ya kusisitiza kuwa haiwezi kutoa ushirikiano kwa kamati ambayo haipo kwa mujibu wa sheria, CHADEMA kimeshangazwa na kusudio hilo la Kamati ya Nchimbi kutoa mwaliko wa kutaka kukutana na viongozi wa CHADEMA, huku ikitambua wazi msimamo wa chama hiki juu ya uwepo wa kamati hiyo mara tu ilipoundwa.

Kutoa ushirikiano kwa kamati ambayo haina mamlaka ya kisheria ya kuhakikisha ukweli mtupu unajulikana na haki ionekane ikitendeka kutokana na kifo hicho na vingine vingi ambavyo vimefanywa na Jeshi la Polisi dhidi ya raia wasiokuwa na hatia, kwa masuala mbalimbali yakiwemo ya kisiasa, ni kuhalalisha uvunjivu wa haki za binadamu, Katiba na sheria za nchi. CHADEMA haiko tayari kuona hali hiyo ikifanyika.

Katika kuonesha msisitizo wa kutokubali mwaliko wa Kamati ya Nchimbi inayotaka kutafakari matukio ya vifo ambapo Jeshi la Polisi limewanyang’anya watu wasio na hatia haki ya kuishi, katika barua yake ya majibu, CHADEMA pia kimeambatanisha nakala ya barua ya tarehe 10/09/2012 iliyowasilishwa kwa Rais, ili kamati hiyo iweze kuelewa msimamo mpana wa chama kuhusu mauaji ya kisiasa yanayofanyika nchini.

Kwa taarifa hii, CHADEMA kinaendelea kusisitiza maazimio ya Kamati Kuu ya Chama, ambayo pamoja na mambo mengine, iliazimia kuwa kutokana na mfululizo wa matukio ya mauaji ya kisiasa yanayofanywa na Jeshi la Polisi katika shughuli halali za chama, Waziri wa Mambo ya Ndani Emmanuel Nchimbi, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Said Mwema, Mkuu wa Operesheni wa Jeshi la Polisi Paul Chagonja na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile wawajibike kwa kujiuzulu au Rais awawajibishe kwa kuwafukuza kazi ili wapishe uchunguzi huru na wa haki.

Pia Kamanda wa Polisi Iringa, Michael Kamuhanda, Kamanda wa FFU Mkoa wa Morogoro, na askari wote wanaoonekana kwenye picha wakiwa wamemzunguka Mwangosi muda mfupi kabla hajalipuliwa na kuuwawa, wakamatwe haraka na kushtakiwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya Mwangosi. Kinyume na hapo ni kuchezea akili za wapenda haki na uwajibikaji, ikiwa moja ya misingi ya amani Tanzania na dunia nzima kwa ujumla.

CHADEMA inapenda kusisitiza kuwa itatoa ushirikiano kwa chombo kitachoundwa kwa mujibu wa Sheria huku ikitilia msisitizo wito kwa Rais kuunda Tume ya Kimahakama/Kijaji kuchunguza vifo vyote vyenye utata na vinavyohusishwa na masuala ya kisiasa kama tulivyopendekeza kwake hapo kabla.

Imetolewa leo Septemba 24, 2012 Dar es Salaam na;

Tumaini Makene
Ofisa Habari wa CHADEMA

Tuesday, September 18, 2012

Hoteli ya kwanza kwa ubora Duniani iko Tanzania



Photo: Courtesy of Singita Grumeti Reserves

Kwa mwaka wa pili mfululizo, hoteli bora duniani ipo Tanzania.

Aidha, kati ya hoteli bora duniani 20, Tanzania ina tatu kwa jumla ikiwemo hiyo ya 1, 9 na ya 15.

Kenya wana moja tu kwenye nafasi ya 20 na Afrika Kusini ina nne, nafasi ya 7, 10, 13, na 14.

Baada ya hoteli hizi, kuna moja tu ya Afrika huko Botswana kwenye nafasi ya 17.

Bofya hapa http://www.travelandleisure.com/worldsbest/2012/hotels
kuziona zote 100 lakini kwa chini hapo kuna orodha ya 20 za kwanza.....................
 
Top 100 Hotels Overall
Rank
'11
Name
Score
1
1
Singita Grumeti Reserves, Serengeti National Park, Tanzania T+L Find
98.25
2
6
Triple Creek Ranch, Darby, Montana
98.22
3
-
Southern Ocean Lodge, Kangaroo Island, Australia DebutT+L Find
97.87
4
5
Oberoi Udaivilas, Udaipur, India
97.50
5
55
Discovery Shores, Boracay, Phillippines
96.77
6
-
Nayara Hotel, Spa & Gardens, La Fortuna-Arenal, Costa Rica Debut
96.36
7
39
96.33
8
19
96.12
9
-
95.85
10
2
Singita Sabi Sand, Kruger National Park Area, South Africa
95.74
11
40
The Peninsula, Bangkok Hall of Fame
95.72
12
-
Wentworth Mansion, Charleston, South Carolina
95.47
13
-
Sabi Sabi Private Game Reserve Lodges, Kruger National Park Area, South Africa
95.40
14
-
One&Only, Cape Town T+L Find
95.33
15
9
Kirawira Luxury Tented Camp, Serengeti National Park, Tanzania
95.27
16
11
The Lodge at Kauri Cliffs, North Island, New Zealand
95.25
17
20
Mombo Camp and Little Mombo Camp, Moremi Game Reserve, Botswana
95.17
18
23
95.04
19
-
Tu Tu'tun Lodge, Gold Beach, Oregon
95.00
20
67
Fairmont Mara Safari Club, Masai Mara, Kenya
94.84



Hata hivyo, nchi yetu inazungukwa mara kumi hadi kumi na moja na jirani zetu Kenya kwenye pato la utalii na pia hoteli za Kenya ziliopo pwani tu, zinazidi kwa idadi jumla ya hoteli zote zilizopo Tanzania Bara.



Singita Grumeti Reserves 
 

Photo: Courtesy of Singita Grumeti Reserves
Sasakwa
Serengeti Plains
Serengeti National Park, Tanzania
TEL: 27 21 683-3424
TEL: +1 770 947 7049/98
South Africa’s pioneering Singita tourism group revamped a pair of lavish lodges and a tented camp in the Grumeti Reserves of Serengeti National Park. You almost expect to see Teddy Roosevelt behind the wheel of one of the two vintage Chevrolets parked at the entrance to Sabora, a safari camp accessorized with antique mahogany chests, worn-leather folding chairs, and thick Persian rugs. Faru Faru, with six chalets overlooking the Grumeti River, channels a Swahili beach resort; a swimming pool curves in front of an open-air lounge, where guests sip sunset cocktails as elephants gather at the watering hole below. The reserve’s flagship is Sasakwa, an East African ranch house set on a plateau with panoramic views of the plains. The lodge’s wood-paneled libraries have an English country club feel, and there are seven cottage residences, each with a garden and plunge pool. Tennis courts, a spa, and a yoga center occupy guests between twice-daily game drives, where sightings include wildebeest, zebras, and gazelles.